لَّوۡ أَرَادَ ٱللَّهُ أَن يَتَّخِذَ وَلَدٗا لَّٱصۡطَفَىٰ مِمَّا يَخۡلُقُ مَا يَشَآءُۚ سُبۡحَٰنَهُۥۖ هُوَ ٱللَّهُ ٱلۡوَٰحِدُ ٱلۡقَهَّارُ
Lau kuwa Mwenyezi Mungu angeli taka kuwa na mwana, basi bila ya shaka angeli teua amtakaye katika alio waumba. Subhanahu, Ametakasika na hayo! Yeye ni Mwenyezi Mungu Mmoja, Mtenda atakalo.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Lau Angalitaka Mwenyezi Mungu kuwa na mtoto, Angalichagua, miongoni mwa viumbe Vyake, Anachotaka. Ameepukana Mwenyezi Mungu na kutakasika na kuwa na mtoto! Hakika Yeye ni Mmoja Aliye Pekee na kupwekeka, Mwenye kutegemewa kwa kila haja, Mwenye kutendesha nguvu ambaye Amewalazimisha viumbe kwa uweza Wake, basi kila kitu kinamdhalilikia Yeye na kumnyenyekea.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس