وَإِن تُكَذِّبُواْ فَقَدۡ كَذَّبَ أُمَمٞ مِّن قَبۡلِكُمۡۖ وَمَا عَلَى ٱلرَّسُولِ إِلَّا ٱلۡبَلَٰغُ ٱلۡمُبِينُ
Na mkikadhibisha, basi kaumu kadhaa wa kadhaa za kabla yenu zilikwisha kadhibisha. Na si juu ya Mtume ila kufikisha Ujumbe waziwazi.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Na mkimkanusha, enyi watu, Mtume wetu Muhammad, rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukiye, katika kile alichowalingania mkifuate cha kumuabudu Mwenyezi Mungu Peke Yake, basi kuna makundi ya watu kabla yenu waliowakanusha Mitume wao katika kile walichowaitia, na kwa hivyo zikawashukia hasira za Mwenyezi Mungu. Na Mtume Muhammad hana jukumu lingine isipokuwa ni kuwafikishia nyinyi kutoka kwa Mwenyezi Mungu ujumbe Wake ufikishaji wenye uwazi, na ashafanya hilo.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس