وَمَن يُطِعِ ٱللَّهَ وَرَسُولَهُۥ وَيَخۡشَ ٱللَّهَ وَيَتَّقۡهِ فَأُوْلَـٰٓئِكَ هُمُ ٱلۡفَآئِزُونَ
Na wenye kumt'ii Mwenyezi Mungu na Mtume wake, na wakamwogopa Mwenyezi Mungu na wakamcha, basi hao ndio wenye kufuzu.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Na mwenye kumtii Mwenyezi Mungu na Mtume Wake katika kufuata maamrisho na kujiepusha na makatazo na akaogopa mwisho mbaya wa uasi na akajihadhari na adhabu ya Mwenyezi Mungu, basi hao ndio wenye kufuzu kupata neema Peponi..
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس