وَأَصۡحَٰبُ مَدۡيَنَۖ وَكُذِّبَ مُوسَىٰۖ فَأَمۡلَيۡتُ لِلۡكَٰفِرِينَ ثُمَّ أَخَذۡتُهُمۡۖ فَكَيۡفَ كَانَ نَكِيرِ
Na watu wa Madiana. Na Musa pia alikanushwa. Nikawapa muda makafiri, kisha nikawatia mkononi. Basi ilikuwaje adhabu yangu!
Ali Muhsin Al - Swahili translation
na watu wa Madyan waliomkanusha Shu'ayb na pia Fir'awn na watu wake walimkanusha Mūsā. Sikuwaharakishia ummah hao mateso, bali niliwapa muda kisha kila mmoja wa hao niliupatiliza kwa adhabu. Ilikuwaje vile nilivyowakataza wao ukafiri wao na ukanushaji wao na nilivyowabadilishia neema waliokuwa nayo kwa adhabu na maangamivu?
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس