وَٱلَّذِينَ يَرۡمُونَ ٱلۡمُحۡصَنَٰتِ ثُمَّ لَمۡ يَأۡتُواْ بِأَرۡبَعَةِ شُهَدَآءَ فَٱجۡلِدُوهُمۡ ثَمَٰنِينَ جَلۡدَةٗ وَلَا تَقۡبَلُواْ لَهُمۡ شَهَٰدَةً أَبَدٗاۚ وَأُوْلَـٰٓئِكَ هُمُ ٱلۡفَٰسِقُونَ
Na wanao wasingizia wanawake mahashumu, kisha wasilete mashahidi wane, basi watandikeni bakora thamanini, na msiwakubalie ushahidi wao tena. Na hao ndio wapotovu.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Na wale wanaowatuhumu watu waliojihifidhi, miongoni mwa wanaume na wanawake, kwa uchafu wa uzinifu pasi na kushuhudia pamoja na wao mashahidi wanne waadilifu, basi wapigeni mboko themanini na msiwakubalie ushahidi mwingine wowote kabisa, na hao ndio waliotoka nje ya utiifu wa Mwenyezi Mungu.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس