أَلَآ إِنَّهُمۡ يَثۡنُونَ صُدُورَهُمۡ لِيَسۡتَخۡفُواْ مِنۡهُۚ أَلَا حِينَ يَسۡتَغۡشُونَ ثِيَابَهُمۡ يَعۡلَمُ مَا يُسِرُّونَ وَمَا يُعۡلِنُونَۚ إِنَّهُۥ عَلِيمُۢ بِذَاتِ ٱلصُّدُورِ
Hebu angalia! Ati wanafunika vilivyomo vifuani mwao ili wamfiche Mwenyezi Mungu! Jueni kuwa wanapo jigubika nguo zao Yeye anajua wanayo yaficha na wanayo yatangaza. Hakika Yeye ni Mjuzi wa yaliyomo vifuani.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Hakika washirikina hawa wanaficha ukafiri katika nyoyo zao wakidhani kwamba yale ambayo nafsi zao zinayadhamiria yanafichika kwa Mwenyezi Mungu. Kwani hawajui wanapoifinika miili yao kwa nguo zao kwamba hayafichiki kwa Mwenyezi Mungu mambo yao ya siri na ya wazi? Hakika Yeye ni Mjuzi wa kila ambacho vifua vyao vinakifinika miongoni mwa nia, madhamirio na siri.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس