ٱلَّذِينَ يَصُدُّونَ عَن سَبِيلِ ٱللَّهِ وَيَبۡغُونَهَا عِوَجٗا وَهُم بِٱلۡأٓخِرَةِ هُمۡ كَٰفِرُونَ
Ambao wanazuilia Njia ya Mwenyezi Mungu, na wanaitakia ipotoke, na wanaikataa Akhera.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Hawa madhalimu ni wale ambao wanawazuia watu na njia ya Mwenyezi Mungu yenye kupelekea kumuubudu na wanataka njia hizi ziwe kombo ziambatane na matamanio yao na wao wanaikanusha Akhera, hawaamini kufufuliwa wa kulipwa.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس