وَمَن يَهۡدِ ٱللَّهُ فَمَا لَهُۥ مِن مُّضِلٍّۗ أَلَيۡسَ ٱللَّهُ بِعَزِيزٖ ذِي ٱنتِقَامٖ
Na ambaye Mwenyezi Mungu anamwongoa hana wa kumpotoa. Je! Mwenyezi Mungu si Mwenye nguvu anaye weza kulipiza?
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Na yoyote yule ambaye Mwenyezi Mungu Amemuafikia kumuamini Yeye na kufanya matendo yanayoambatana na Kitabu Chake na kumfuata Mtume Wake, basi huyo hana mwenye kumpoteza na kumpotosha na haki ambayo amesimama nayo. Kwani Mwenyezi Mungu si Mshindi katika kuwatesa viumbe Wake waliomkufuru na wale waliomuasi?
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس