وَإِن يُكَذِّبُوكَ فَقَدۡ كَذَّبَ ٱلَّذِينَ مِن قَبۡلِهِمۡ جَآءَتۡهُمۡ رُسُلُهُم بِٱلۡبَيِّنَٰتِ وَبِٱلزُّبُرِ وَبِٱلۡكِتَٰبِ ٱلۡمُنِيرِ
Na wakikukanusha basi walikwisha wakanusha walio kuwa kabla yao. Mitume wao waliwajia kwa dalili wazi wazi na kwa maandiko na Kitabu chenye nuru.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Na wanapokukanusha washirikina hawa , basi wale waliopita kabla yao waliwakanusha Mitume wao ambao waliwajia na miujiza iliyo wazi yenye kutolea ushahidi unabii wao, na waliwajia na Vitabu, ambavyo ndani yake zimekusanywa hukumu nyingi, na (waliwajia na) Kitabu chenye kutoa mwangaza chenye kubainisha njia ya kheri na shari.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس