وَمَا لَهُمۡ أَلَّا يُعَذِّبَهُمُ ٱللَّهُ وَهُمۡ يَصُدُّونَ عَنِ ٱلۡمَسۡجِدِ ٱلۡحَرَامِ وَمَا كَانُوٓاْ أَوۡلِيَآءَهُۥٓۚ إِنۡ أَوۡلِيَآؤُهُۥٓ إِلَّا ٱلۡمُتَّقُونَ وَلَٰكِنَّ أَكۡثَرَهُمۡ لَا يَعۡلَمُونَ
Lakini wana jambo gani hata Mwenyezi Mungu asiwaadhibu, na hali ya kuwa wanawazuilia watu Msikiti Mtakatifu? Wala wao hawakuwa ndio walinzi wake, bali walinzi wake hawakuwa ila wacha-Mngu tu. Lakini wengi katika wao hawajui.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Na vipi wao wasistahili adhabu ya Mwenyezi Mungu na hali wao wanawazuia mawalii wake Waumini kutufu Alkaba na kuswali ndani ya msikiti wa H(arām. Na wao hawakuwa ni mawalii wa Mwenyezi Mungu. Mawalii Wake si wengine isipokuwa wale wanaomuogopa Yeye kwa kutekeleza faradhi Alizoziweka na kujiepusha na mambo ya kumuasi. Lakini wengi zaidi wa makafiri hawajui, na kwa hivyo walidai kwamba wana jambo ambalo wasiokuwa wao wana haki nalo zaidi.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس