وَلَوۡ نَشَآءُ لَأَرَيۡنَٰكَهُمۡ فَلَعَرَفۡتَهُم بِسِيمَٰهُمۡۚ وَلَتَعۡرِفَنَّهُمۡ فِي لَحۡنِ ٱلۡقَوۡلِۚ وَٱللَّهُ يَعۡلَمُ أَعۡمَٰلَكُمۡ
Na tungeli penda tungeli kuonyesha hao na ungeli watambua kwa alama zao; lakini bila ya shaka utawajua kwa namna ya msemo wao. Na Mwenyezi Mungu anavijua vitendo vyenu.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Na lau tungalitaka, ewe Nabii, tungalikuonesha hao watu wenyewe, ukawatambua kwa alama zilizo wazi kwao. Na kwa hakika utawajua kutokana na maneno yao yaliyodhihirika yenye kuonyesha malengo yao. Na kwa Mwenyezi Mungu, Aliyetukuka, hakuna chochote kinachofichamana cha matendo ya wanaomtii wala matendo ya wanaomuasi, na Atamlipa kila mmoja kwa anachostahili.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس