وَإِن تَوَلَّوۡاْ فَٱعۡلَمُوٓاْ أَنَّ ٱللَّهَ مَوۡلَىٰكُمۡۚ نِعۡمَ ٱلۡمَوۡلَىٰ وَنِعۡمَ ٱلنَّصِيرُ
Na kama wakigeuka basi jueni kwamba Mwenyezi Mungu ndiye Mola wenu, ni Mola Mwema na Msaidizi Mwema.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Na wakiyapa mgongo hawa washirikina yale mliyowaitia, enyi Waumini, ya kumuamini Mwenyezi Mungu na Mtume Wake na kuacha kuwapiga vita nyinyi, na wakakataa isipokuwa kuendelea kwenye ukafiri na kuwapiga vita nyinyi, basi kuweni na yakini kwamba Mwenyezi Mungu ni Mwenye kuwasaidia na kuwapa ushindi juu yao. Yeye Ndiye bora wa kuwasaidia na kuwapa nyinyi ushindi na wale wenye kujitegemeza Kwake juu ya maadui zenu.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس