إِنَّ ٱلَّذِينَ كَفَرُواْ وَصَدُّواْ عَن سَبِيلِ ٱللَّهِ ثُمَّ مَاتُواْ وَهُمۡ كُفَّارٞ فَلَن يَغۡفِرَ ٱللَّهُ لَهُمۡ
Hakika walio kufuru na wakazuilia njia ya Mwenyezi Mungu, kisha wakafa na hali ni makafiri, Mwenyezi Mungu hatawasamehe makosa yao.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Hakika ya wale waliokataa kuwa Mwenyezi Mungu Ndiye Mola wa haki Peke Yake Asiye na mshirika na wakawazuia watu na Dini Yake, kisha wakafa wakiwa katika hali hiyo, Mwenyezi Mungu Hatawasamehe, na Atawapa adhabu ikiwa ndio mateso yao kwa ukanushaji wao, na Atawafedhehesha mbele ya halaiki ya watu.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس