وَإِن يُكَذِّبُوكَ فَقَدۡ كُذِّبَتۡ رُسُلٞ مِّن قَبۡلِكَۚ وَإِلَى ٱللَّهِ تُرۡجَعُ ٱلۡأُمُورُ
Na wakikukanusha, basi walikwisha kanushwa Mitume kabla yako. Na mambo yote yatarudishwa kwa Mwenyezi Mungu.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Na watu wako wakikukanusha, ewe Mtume, kwa hakika wamekanushwa Mitume kabla yako wewe. Na kwa Mwenyezi Mungu mambo yanaishia huko Akhera, basi hapo Atamlipa kila mmoja anachostahili. Katika hii pana kumliwaza Mtume, rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس