وَٱلَّذِيٓ أَوۡحَيۡنَآ إِلَيۡكَ مِنَ ٱلۡكِتَٰبِ هُوَ ٱلۡحَقُّ مُصَدِّقٗا لِّمَا بَيۡنَ يَدَيۡهِۗ إِنَّ ٱللَّهَ بِعِبَادِهِۦ لَخَبِيرُۢ بَصِيرٞ
Na hayo tuliyo kufunulia kutoka Kitabuni ni Kweli yenye kusadikisha yaliyo kuwa kabla yake. Hakika Mwenyezi Mungu kwa waja wake ni Mwenye khabari na Mwenye kuona.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Na Qur’ni tuliyokuteremshia wewe, ewe Mtume, ndiyo haki inayosadikisha Vitabu Alivyoviteremsha Mwenyezi Mungu kwa Mitume Wake kabla yako. Hakika Mwenyezi Mungu ni Mtambuzi wa mambo ya waja Wake, ni Mwenye kuviona vitendo vyao, na Atawalipa wema kwa hayo.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس