أَفۡتَرَىٰ عَلَى ٱللَّهِ كَذِبًا أَم بِهِۦ جِنَّةُۢۗ بَلِ ٱلَّذِينَ لَا يُؤۡمِنُونَ بِٱلۡأٓخِرَةِ فِي ٱلۡعَذَابِ وَٱلضَّلَٰلِ ٱلۡبَعِيدِ
Ama amemzulia Mwenyezi Mungu uwongo, au ana wazimu. Bali wasio amini Akhera wamo adhabuni na upotofu wa mbali kabisa.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Kwani mtu huyu amemzulia Mwenyezi Mungu urongo, au ana wazimu na kwa hivyo anasema jambo asilolijua? Mambo si vile kama wanavyosema makafiri, bali Muhammad ni mkweli wa wakweli. Na wale wasioamini kufufuliwa na wasiofanya matendo ya kuwafaa huko, watakuwa kwenye adhabu ya milele huko Akhera, na wako kwenye upotevu wa mbali hapa duniani.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس