قُلۡ إِنَّ رَبِّي يَقۡذِفُ بِٱلۡحَقِّ عَلَّـٰمُ ٱلۡغُيُوبِ
Sema: Hakika Mola wangu Mlezi anaondoa upotovu kwa Haki. Yeye ndiye Mwenye kujua vyema yaliyo ghaibu.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Sema, ewe Mtume, umwambie anayekanusha upwekeshaji wa Mwenyezi Mungu na ujumbe wa Uislamu, «Hakika Mola wangu Anauvurumiza ubatilifu kwa hoja za ukweli, hivyo basi ukaufedhehi na ukauangamiza. Na Mwenyezi Mungu ni Mjuzi mno wa vitu visivyoonekana, hakuna kinachofichamana Kwake chochote ardhini na mbinguni.»
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس