قَالَ يَـٰٓأَيُّهَا ٱلۡمَلَؤُاْ أَيُّكُمۡ يَأۡتِينِي بِعَرۡشِهَا قَبۡلَ أَن يَأۡتُونِي مُسۡلِمِينَ
Akasema: Enyi wahishimiwa! Ni nani kati yenu atakaye niletea kiti chake cha enzi kabla hawajanijia nao wamekwisha salimu amri.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Sulaymān akasema akiwahutubia wale ambao Mwenyezi Mungu Amemdhalilishia miongoni mwa majini na binadamu, «Ni nani kati yenu ataniletea kitanda cha ufalme wake kabla hawajanijia wakiwa katika hali ya kufuata na kutii?»
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس