وَلَوۡ أَنَّهُمۡ رَضُواْ مَآ ءَاتَىٰهُمُ ٱللَّهُ وَرَسُولُهُۥ وَقَالُواْ حَسۡبُنَا ٱللَّهُ سَيُؤۡتِينَا ٱللَّهُ مِن فَضۡلِهِۦ وَرَسُولُهُۥٓ إِنَّآ إِلَى ٱللَّهِ رَٰغِبُونَ
Na laiti wao wangeli ridhia kile alicho wapa Mwenyezi Mungu na Mtume wake, na wakasema: Mwenyezi Mungu anatutosheleza, Mwenyezi Mungu atatupa katika fadhila yake - na pia Mtume wake; hakika sisi ni wenye kumtaka Mwenyezi Mungu!
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Na lau hawa wanaokutia kombo katika ugawaji wa sadaka waliridhika na kile ambacho Mwenyezi Mungu na Mtume Wake waliwagawia na wakasema, «Mwenyezi Mungu Ndiye Anayetutosha. Mwenyezi Mungu Atatupa kutokana na nyongeza Zake, na Mtume Wake atatupa kutokana na kile Mwenyezi Mungu Alichompa. Sisi tuna hamu Mwenyezi Mungu Atukunjulie na Atukwasishe tusihitajie sadaka wala tusichukue sadaka za watu.» Lau walifanya hivyo, ingalikuwa bora na yenye manufaa zaidi kwao.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس