يَوۡمَ يُحۡمَىٰ عَلَيۡهَا فِي نَارِ جَهَنَّمَ فَتُكۡوَىٰ بِهَا جِبَاهُهُمۡ وَجُنُوبُهُمۡ وَظُهُورُهُمۡۖ هَٰذَا مَا كَنَزۡتُمۡ لِأَنفُسِكُمۡ فَذُوقُواْ مَا كُنتُمۡ تَكۡنِزُونَ
Siku zitapo tiwa moto katika Moto wa Jahannamu, na kwazo vikachomwa vipaji vya nyuso zao na mbavu zao na migongo yao, wakaambiwa: Haya ndiyo mlio jilimbikia nafsi zenu, basi onjeni mliyo kuwa mkilimbika.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Siku ya Kiyama yatawekwa mapande ya dhahabu na fedha kwenye Moto, na yataposhika moto sana, watachomwa nayo, hao wenyewe, nyuso zao, mbavu zao na migongo yao. Na wataambiwa kwa kuwaumbua, «Haya ndiyo mali yenu mliyoyakumbatia na mkazuia, katika mali hayo, haki za Mwenyezi Mungu. Basi onjeni adhabu iumizayo, kwa sababu ya kukusanya kwenu na kuzuia.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس