لَقَدۡ جَآءَكُمۡ رَسُولٞ مِّنۡ أَنفُسِكُمۡ عَزِيزٌ عَلَيۡهِ مَا عَنِتُّمۡ حَرِيصٌ عَلَيۡكُم بِٱلۡمُؤۡمِنِينَ رَءُوفٞ رَّحِيمٞ
Hakika amekwisha kujieni Mtume kutokana na nyinyi wenyewe; yanamhuzunisha yanayo kutaabisheni; anakuhangaikieni sana. Kwa Waumini ni mpole na mwenye huruma.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Hakika amewajia nyinyi, enyi Waumini, mjumbe atokanao na watu wenu, Azionea uzito shida mlizonazo na masumbuko, ana pupa kwamba muamini na mambo yenu yafaulu na yeye kwa Waumini ni mwingi wa upole na huruma.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس