وَإِذَا مَآ أُنزِلَتۡ سُورَةٞ فَمِنۡهُم مَّن يَقُولُ أَيُّكُمۡ زَادَتۡهُ هَٰذِهِۦٓ إِيمَٰنٗاۚ فَأَمَّا ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ فَزَادَتۡهُمۡ إِيمَٰنٗا وَهُمۡ يَسۡتَبۡشِرُونَ
Na inapo teremshwa Sura wapo miongoni mwao wasemao: Ni nani miongoni mwenu Sura hii imemzidishia Imani? Ama wale walio amini inawazidishia Imani, nao wanafurahi.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Na pindi Mwenyezi Mungu Aiteremshapo sura, miongoni mwa sura za Qur’ani, kwa Mtume Wake, basi kati ya hawa wanafiki kuna wanaosema, kwa kukanusha na kufanya shere, «Ni nani wenu ambaye sura hii ilimfanya imani yake, kwa Mwenyezi Mungu na aya Zake, iongezeke? Basi wale waliomuamini Mwenyezi Mungu na Mtume Wake,, kule kuteremka sura, kuliwaongezea waolmani kwa kuijua na kuizingatia na kuiamini na kuitumia, na hali wao wanafurahia Imani na yakini Alizowapa Mwenyezi Mungu.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس