وَمَا لَنَا لَا نُؤۡمِنُ بِٱللَّهِ وَمَا جَآءَنَا مِنَ ٱلۡحَقِّ وَنَطۡمَعُ أَن يُدۡخِلَنَا رَبُّنَا مَعَ ٱلۡقَوۡمِ ٱلصَّـٰلِحِينَ
Na kwa nini tusimuamini Mwenyezi Mungu na Haki iliyo tujia, na hali tunatumai Mola wetu Mlezi atuingize pamoja na watu wema?
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Na walisema, «Kwani tuna lawama gani sisi kwa kumuamini kwetu Mwenyezi Mungu, kuikubali haki ambayo alikuja nayo kwetu Muhammad , rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie, kutoka kwa Mwenyezi Mungu na kumfuata kwetu yeye, na hali tunatumai kuwa Mola wetu Atatutia kwenye Pepo Yake, Siku ya Kiyama, pamoja na walio watiifu Kwake?»
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس