إِنَّ ٱلَّذِينَ يُنَادُونَكَ مِن وَرَآءِ ٱلۡحُجُرَٰتِ أَكۡثَرُهُمۡ لَا يَعۡقِلُونَ
Hakika hao wanao kuita nawe uko nyuma ya vyumba, wengi wao hawana akili.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Hakika ya wale wanaokuita, ewe Nabii, nyuma ya vyumba vyako kwa sauti ya juu, wengi wao hawana akili ya kuwapelekea kuwa na adabu nzuri pamoja na Mtume wa Mwenyezi Mungu, rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie, na kumheshimu.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس