وَمَا ٱخۡتَلَفۡتُمۡ فِيهِ مِن شَيۡءٖ فَحُكۡمُهُۥٓ إِلَى ٱللَّهِۚ ذَٰلِكُمُ ٱللَّهُ رَبِّي عَلَيۡهِ تَوَكَّلۡتُ وَإِلَيۡهِ أُنِيبُ
Na mkikhitalifiana katika jambo lolote, basi hukumu yake iko kwa Mwenyezi Mungu. Huyo Mwenyezi Mungu ndiye Mola wangu Mlezi, ninaye mtegemea na kwake Yeye narejea.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Na kitu chochote kile mnachotafautiana kwacho , enyi watu, miongoni mwa mambo ya dini yenu, basi hukumu irudishwe kwa Mwenyezi Mungu katika Kitabu Chake na Sunnah ya Mtume Wake, rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie. Huyo Ndiye Mwenyezi Mungu, Mola wangu na Mola wenu, Kwake Yeye nimetegemea katika mambo yangu, na Kwake Yeye ninarejea katika hali zangu zote.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس