فَٱتَّقُواْ ٱللَّهَ مَا ٱسۡتَطَعۡتُمۡ وَٱسۡمَعُواْ وَأَطِيعُواْ وَأَنفِقُواْ خَيۡرٗا لِّأَنفُسِكُمۡۗ وَمَن يُوقَ شُحَّ نَفۡسِهِۦ فَأُوْلَـٰٓئِكَ هُمُ ٱلۡمُفۡلِحُونَ
Basi mcheni Mwenyezi Mungu kama mwezavyo, na sikieni, na t'iini, na toeni, itakuwa kheri kwa nafsi zenu. Na mwenye kuepushwa na uchoyo wa nafsi yake, basi hao ndio walio fanikiwa.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Fanyeni juhudi zenu, enyi Waumini, na tumieni nguvu zenu katika kumcha Mwenyezi Mungu, na msikilizeni Mtume wa Mwenyezi Mungu, rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie, usikilizaji wa kuzingatia na kufikiri, zifuateni amri Zake na myaepuke makatazo Yake na mtoe katika kile Alichowaruzuku Mwenyezi Mungu, hilo litakuwa bora kwenu. Na atakayeepukana na uchoyo na kubania kilichozidi katika mali, basi hao ndio watakaozipata kheri zote, watakaofaulu kupata kila wanalolitaka.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس