مَآ أَصَابَ مِن مُّصِيبَةٍ إِلَّا بِإِذۡنِ ٱللَّهِۗ وَمَن يُؤۡمِنۢ بِٱللَّهِ يَهۡدِ قَلۡبَهُۥۚ وَٱللَّهُ بِكُلِّ شَيۡءٍ عَلِيمٞ
Haufiki msiba wowote ila kwa idhini ya Mwenyezi Mungu. Na mwenye kumuamini Mwenyezi Mungu huuongoa moyo wake. Na Mwenyezi Mungu ni Mjuzi wa kila kitu.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Halimpati yoyote jambo lolote la shida isipokuwa kwa ruhusa ya Mwenyezi Mungu na mapitisho Yake na makadirio Yake. Na yoyote anayemuamini Mwenyezi Mungu, Atauongoza moyo Wake ufuate amri Zake na uridhike na mapitisho Yake. Atauongoza kwenye njia nzuri ya maneno, vitendo na hali. Kwani uongofu hasa ni wa moyo, na viungo vinafuata. Na Mwenyezi Mungu kwa kila kitu ni Mjuzi, hakifichamani Kwake chochote miongoni mwa hivyo.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس