يُرِيدُونَ لِيُطۡفِـُٔواْ نُورَ ٱللَّهِ بِأَفۡوَٰهِهِمۡ وَٱللَّهُ مُتِمُّ نُورِهِۦ وَلَوۡ كَرِهَ ٱلۡكَٰفِرُونَ
Wanataka kuizima nuru ya Mwenyezi Mungu kwa vinywa vyao. Na Mwenyezi Mungu atakamilisha nuru yake ijapo kuwa makafiri watachukia.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Hawa madhalimu wanataka kuitangua haki aliyotumilizwa kwayo Muhammad, rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie, nayo ni Qur’ani, kwa maneno yao ya urongo. Na Mwenyezi Mungu ni Mwenye kuipa nguvu haki kwa kuitimiza Dini Yake japokuwa wale wapingaji wenye kukanusha watachukia.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس