كَمَثَلِ ٱلَّذِينَ مِن قَبۡلِهِمۡ قَرِيبٗاۖ ذَاقُواْ وَبَالَ أَمۡرِهِمۡ وَلَهُمۡ عَذَابٌ أَلِيمٞ
Ni kama mfano wa walio kuwa kabla yao hivi karibuni. Walionja uovu wa mambo yao. Nao watapata adhabu iliyo chungu.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Mfano wa hawa Mayahudi kwa mateso yaliyowashukia ni kama mfano wa makafiri wa Kikureshi siku ya Badr na Mayahudi wa Banū Qaynuqā'kwa kuwa walionja mwisho mbaya wa ukafiri wao na uadui wao kwa Mtume, rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie, duniani, na huko Akhera watapata adhabu kali yenye uchungu.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس