وَأَطِيعُواْ ٱللَّهَ وَأَطِيعُواْ ٱلرَّسُولَۚ فَإِن تَوَلَّيۡتُمۡ فَإِنَّمَا عَلَىٰ رَسُولِنَا ٱلۡبَلَٰغُ ٱلۡمُبِينُ
Na mt'iini Mwenyezi Mungu, na mt'iini Mtume. Mkigeuka, basi hakika juu ya Mtume wetu ni kufikisha (Ujumbe wake) kwa uwazi tu.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Na mtiini Mwenyezi Mungu, enyi watu, na muongokee Kwake katika yale Aliyoyaamrisha na Aliyoyakataza, na mfuateni Mtume, rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie, katika yale aliyowafikishia kutoka kwa Mola wake. Na iwapo mtaupa mgongo utiifu wenu kwa Mwenyezi Mungu na Mtume Wake, basi Mjumbe wetu hana madhara yoyote kutokana na kupa mgongo kwenu. Jukumu lake yeye ni kuwafikishia nyinyi yale Aliyotumilizwa kwayo ufikishaji wenye maelezo ya waziwazi.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس