لَهُۥ مُلۡكُ ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَٱلۡأَرۡضِۖ يُحۡيِۦ وَيُمِيتُۖ وَهُوَ عَلَىٰ كُلِّ شَيۡءٖ قَدِيرٌ
Yeye ndiye Mwenye ufalme wa mbingu na ardhi. Anahuisha na anafisha. Na Yeye ni Mwenye uweza wa kila kitu.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Ni Yake mamlaka ya mbinguni na ardhini na vilivyomo ndani yake. Yeye Ndiye Mmiliki Mwenye kuendesha mambo ya viumbe Vyake, Anahuisha na kufisha, na Yeye juu ya kila kitu ni Muweza, hakuna kinachomshinda Akikitaka kifanyike, Anachokitaka kinakuwa, na Asichokitaka hakiwi.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس