لَّا تَجِدُ قَوۡمٗا يُؤۡمِنُونَ بِٱللَّهِ وَٱلۡيَوۡمِ ٱلۡأٓخِرِ يُوَآدُّونَ مَنۡ حَآدَّ ٱللَّهَ وَرَسُولَهُۥ وَلَوۡ كَانُوٓاْ ءَابَآءَهُمۡ أَوۡ أَبۡنَآءَهُمۡ أَوۡ إِخۡوَٰنَهُمۡ أَوۡ عَشِيرَتَهُمۡۚ أُوْلَـٰٓئِكَ كَتَبَ فِي قُلُوبِهِمُ ٱلۡإِيمَٰنَ وَأَيَّدَهُم بِرُوحٖ مِّنۡهُۖ وَيُدۡخِلُهُمۡ جَنَّـٰتٖ تَجۡرِي مِن تَحۡتِهَا ٱلۡأَنۡهَٰرُ خَٰلِدِينَ فِيهَاۚ رَضِيَ ٱللَّهُ عَنۡهُمۡ وَرَضُواْ عَنۡهُۚ أُوْلَـٰٓئِكَ حِزۡبُ ٱللَّهِۚ أَلَآ إِنَّ حِزۡبَ ٱللَّهِ هُمُ ٱلۡمُفۡلِحُونَ
Huwakuti watu wanao muamini Mwenyezi Mungu na Siku ya Mwisho kuwa wanawapenda wanao mpinga Mwenyezi Mungu na Mtume wake, hata wakiwa ni baba zao, au watoto wao, au ndugu zao, au jamaa zao. Hao ameandika katika nyoyo zao Imani, na amewapa nguvu kwa Roho itokayo kwake. Na atawaingiza katika Mabustani yapitayo mito kati yake. Humo watakaa daima. Mwenyezi Mungu awe radhi nao, na wao wawe radhi naye. Hao ndio Hizbullahi, Kundi la Mwenyezi Mungu. Hakika Kundi la Mwenyezi Mungu ndilo lenye kufanikiwa.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Hutakuta, ewe Mtume, watu wanaomuamini Mwenyezi Mungu na Siku ya Mwisho na wanaofanya matendo waliyoamrishwa na Mwenyezi Mungu, wakiwapenda na kuwategemea wale wanaomsimamishia uadui Mwenyezi Mungu na Mtume Wake na wanaoenda kinyume na amri zao, ingawa ni baba zao au wana wao au ndugu zo au jamaa zao wa karibu. Hao wanaofunga urafiki kwa ajili ya Mwenyezi Mungu na wanaosimamisha uadui kwa ajili Yake ndio wale ambao Mwenyezi Mungu Ameithibitisha Imani ndani ya nyoyo zao na Akawatia nguvu kwa kuwapa ushindi utokao Kwake na msaada dhidi ya adui yao duniani, na Atawaingiza huko Akhera kwenye mabustani ya Peponi ambayo chini ya miti yake inapita mito, hali ya kukaa humo muda mrefu usiomalizika, Amewapa radhi Zake na hatawakasirikia na wao wameridhika na Mola wao kwa yale Aliyowapatia ya utukufu na daraja kubwa. Hao ndio kundi la Mwenyezi Mungu na walioshikana na Yeye, na hao ndio wenye kufaulu kwa kupata furaha ya duniani na Akhera.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس