ٱتَّخَذُوٓاْ أَيۡمَٰنَهُمۡ جُنَّةٗ فَصَدُّواْ عَن سَبِيلِ ٱللَّهِ فَلَهُمۡ عَذَابٞ مُّهِينٞ
Wamefanya viapo vyao ni ngao, na wakaipinga Njia ya Mwenyezi Mungu. Basi hao watapata adhabu ya kufedhehesha.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Wanafiki wameyafanya yale mayamini yao ya urongo ni kinga yao wasipate kuuawa kwa ukafiri wao na kuwazuia Waislamu wasiwapige vita na kuchukua mali yao. Na kwa ajili hiyo wanajizuia wao na kuwazuia wengine njia ya Mwenyezi Mungu, nayo ni Uislamu. Basi watapata adhabu yenye kudhalilisha Motoni kwa kufanya kiburi kwao kwa kujiepusha na kumuamini Mwenyezi Mungu na Mtume Wake na kwa kuzuia kwao njia Yake isifuatwe.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس