أَوَلَمۡ يَرَوۡاْ أَنَّ ٱللَّهَ ٱلَّذِي خَلَقَ ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَٱلۡأَرۡضَ وَلَمۡ يَعۡيَ بِخَلۡقِهِنَّ بِقَٰدِرٍ عَلَىٰٓ أَن يُحۡـِۧيَ ٱلۡمَوۡتَىٰۚ بَلَىٰٓۚ إِنَّهُۥ عَلَىٰ كُلِّ شَيۡءٖ قَدِيرٞ
Je! Hawaoni ya kwamba Mwenyezi Mungu, aliye ziumba mbingu na ardhi, na hakuchoka kwa kuziumba, kuwa ni Muweza wa kuwafufua wafu? Kwani? Hakika Yeye ni Muweza wa kila kitu.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Je, wameghafilika na wasijue kwamba Mwenyezi Mungu, Aliyeumba mbingu na ardhi pasi na mfano uliotangulia na bila kuelemewa na kuziumba, ni Muweza wa kuhuisha wafu ambao Aliwaumba hapo mwanzo? Ndio, hilo ni jambo jepesi kwa Mwenyezi Mungu Aliyetukuka, Ambaye hakuna chochote kinachomshinda. Hakika Yeye kwa kila jambo ni Muweza.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس