أُوْلَـٰٓئِكَ ٱلَّذِينَ نَتَقَبَّلُ عَنۡهُمۡ أَحۡسَنَ مَا عَمِلُواْ وَنَتَجَاوَزُ عَن سَيِّـَٔاتِهِمۡ فِيٓ أَصۡحَٰبِ ٱلۡجَنَّةِۖ وَعۡدَ ٱلصِّدۡقِ ٱلَّذِي كَانُواْ يُوعَدُونَ
Hao ndio tunao wapokelea bora ya vitendo vyao walivyo vitenda, na tunayasamehe makosa yao. Watakuwa miongoni mwa watu wa Peponi. Miadi ya kweli hiyo walio ahidiwa.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Hao ndio ambao tutayapokea kutoka kwao mazuri zaidi ya matendo mema waliyoyafanya, na tutasamehe dhambi zao, wakiwa ni miongoni mwa watu wa Peponi. Ahadi hii tuliyowaahidi ni ahadi ya ukweli na haki isiyokuwa na shaka.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس