وَمِن قَبۡلِهِۦ كِتَٰبُ مُوسَىٰٓ إِمَامٗا وَرَحۡمَةٗۚ وَهَٰذَا كِتَٰبٞ مُّصَدِّقٞ لِّسَانًا عَرَبِيّٗا لِّيُنذِرَ ٱلَّذِينَ ظَلَمُواْ وَبُشۡرَىٰ لِلۡمُحۡسِنِينَ
Na kabla yake kilikuwapo Kitabu cha Musa, kuwa chenye uwongozi na rehema. Na hichi ni Kitabu cha kusadikisha na kilicho kuja kwa lugha ya Kiarabu, ili kiwaonye walio dhulumu, na kiwe ni bishara kwa watendao mema.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Na kabla ya hii Qur’ani, tuliiteremsha Taurati ikiwa ni muongozo kwa Wana wa Isrāīl waiandame na ni rehema kwa wenye kuiamini na kuifuata kivitendo. Na hii Qur’ani inasadikisha Vitabu vilivyokuwa kabla yake. Tumeiteremsha kwa lugha ya Kiarabu ili iwaonye wale waliozidhulumu nafsi zao kwa kukanusha na kuasi. Na bishara njema ni ya wale waliomtii Mwenyezi Mungu na wakafanya wema katika Imani yao na utiifu wao duniani.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس